KWA HABARI ZILIZO HARIRIWA NA KUHAKIKIWA NA WACHAMBUZI MAKINI USIKOSE KUTEMBELEA HAPA KILA SIKU
Sunday, June 3, 2012
WASHINDI WA KILI MUSIC WAFANYA KUFURU VIWANJA VYA POSTA KIJITONYAMA DAR(PICHA KWA HISANI YA BLOG YA DJ CHOKA}
KITOKOLOLO kwa steji
Isha Mashauzi aka Jike la Simba kwa steji
Malkia wa Taarabu Khadija Kopa kwa steji
DJ Mafuvu kutoka EA Radio/TV
AT msanii kutoka ZNZ akilitawala steji
Ben Pol kwa steji
Queen Darling kwa steji
Suma Lee kwa steji...
Saturday, June 2, 2012
kila la heri taifa stars
Leo timu yetu ya Taifa Taifa stars inakipiga na ivory coast katika kuwania nafasi ya kucheza kombe la dunia mwaka 2014 huko brazil
Kwa kufahamu maana ya uzalendo na umuhimu wa mchezo huo wa leo Mwenyekiti wenu naitumia nafasi hii kuitakia kila la heri ili iweze kuipeperusha vema bendera ya Taifa la Tanzania
"mungu ibariki tanzania"
"mungu ibariki taifa stars"
TFF YAWAASA MASHABIKI WA YANGA KUFUATA KANUNI NA TARATIBU ZA KUCHUKUA FOMU ZA UCHAGUZI
WAKATI zoezi la uchukuaji fomu za
kuwania uongozi katika klabu ya Yanga likianza leo, kamati ya uchaguzi ya
Shirikisho la soka Tanzania (TFF) limewataka wanachama wake kufuata kanuni za
uchaguzi zilizowekwa na shirikisho hilo.
Hatua hiyo inafuatia baadhi ya
wanachama wa klabu ya Yanga kukiuka kanuni hizo kwa kutoa taarifa potofu
kuhusiana na uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi za zilizowazi utakaofanyika Julai
15mwaka huu.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya
TFF Deogratius Lyatto alisema jana kwamba uchaguzi huo ni kwa ajili ya kuziba
nafasi za viongozi ili kutimiza akidi na si kwa ajili ya kuchagua upya viongozi
kama inavyoenezwa.
“Kuna upotoshwaji unafanywa na
baadhi ya wanachama kuhusiana na uchaguzi huu, napenda ieleweke kuwa, uchaguzi
huo utajaza nafasi za viongozi waliojiuzulu na ile ya mjumbe mmoja aliyefariki
dunia, hivyo wanachama wa Yanga wafahamu hilo na kuzingatia,”alisema.
Mbali na hilo, Mwenyekiti huyoa
lisema kwamba viongozi watakaochaguliwa watakaa madarakani kwa muda uliosalia
kama katiba inavyoelekeza na kwa mantiki hiyo hiyo viongozi hao watamaliza muda
wao wa miaka minne mwaka 2014.
“TFF inaamini kuwa wajumbe wa kamati
ya uchaguzi wa Yanaga wqatatekeleza wajibu na majukumu yao ya kikatiba na
kikanuni kuhakikisha kwamba klabu hiyo inajaza nafasi zilizowazi katika
mkutanio mu wa uchaguzi kwa kipindi kilichobaki cha mamlaka ya kamati ya
utendaji (ibara ya 29 ya Katiba ya Yanga),”alisema.
Kwa mujibu wa Katibu wa kamati ya
uchaguzi ya Yanga Francis Kaswahili, zoezi la uchukuaji na urejeshaji
fomu litamalizika Juni 6, huku Juni 7 hadi 13 kamati itapitia majina ya
walioomba kugombea na kutangaza majina yao, wakati juni 14 hadi 18 itakuwa ni
kipindi cha kupokea pingamizi.
Aidha, Juni 19 hadi 23 utafanyika
usaili na kutangaza matokeo, wakati juni 24 hadi 26 itakuwa ni kipindi cha
kukata rufaa, juni 27 hadi julao mosi kamati ya uchaguzi TFF itasikiliza rufaa
kama zipo, huku Julai 2 yatatabgazwa majina na kampeni kuanza hadi julai
14.
Uchaguzi huo unafuatia kujiuzulu kwa
aliyekuwa Mwenyekiti Lloyd Nchunga baada ya kushinikizwa na baadhi ya
wanachama wakiongozwa na baraza la wazee wa klabu hiyo kutokana na kushindwa
kuiletea mafanikio klabu hiyo chini ya uongozi wake.
Pia nafasi ya Makamu mwenyekiti
iliyokuwa inashikiliwa na Davis Mosha ambaye alijitoa miezi michache baada ya
kuchaguliwa kutokana na kutoelewana na Nchunga, huku mjumbe Theonest
Rutashoborwa akitangulia mbele ya haki.
Uchaguzi huo pia utajaza nafasi za
Wajumbe walioachia ngazi ambao ni pamoja na Mzee Yusuf, Charles Mgondo na
Ally Mayay.
Kwa sasa Yanga imebaki na wajumbe
wanne, Mohammed Bhinda, Sarah Ramadhan, Tito Osoro na Salum Rupia ambao baada
ya uchaguzi wataungana na viongozi wapya na kuteua wajumbe wengine watatu
kwa mujibu wa katiba, hiyo inatokana na wajumbe hao wa kuteuliwa Seif Ahmed,
Mbaraka Igangula na Pascal Kihanga kujiuzulu.
TAIFA STARS KUIVAA IVORY COASTY USIKU WA LEO HUKU KIM POULSEN AKITAJA KIKOSI MAPEMA
Wachezaji
wa timu ya Soka ya Taifa ‘Taifa Stars’ wakijifua kwenye Uwanja wa wa
kituo cha Michezo mjini Abidjan kujiandaa na mechi ya mchujo ya
Kombe la Dunia dhidi ya Ivory Coast inayotarajiwa kufayika leo kwenye
uwanja wa Felix Houphouet-Boigny.
Kocha
Kim Poulsen ametaja kikosi cha Taifa Stars ambacho leo (Juni 2 mwaka huu)
kitakuwa uwanjani kwenye Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny jijini Abidjan kuivaa
Ivory Coast katika mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia.
Amefanya
mabadiliko katika nafasi mbili kwenye kikosi ambacho Mei 26 mwaka huu kilicheza
mechi ya kujipima nguvu na Malawi (The Flames) iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar
es Salaam na kumalizika kwa suluhu.
Amir
Maftah atacheza beki wa kushoto badala ya Waziri Salum wakati Mrisho Ngasa
atakuwa mmoja kati ya washambuliaji wa mwisho. Ngasa atacheza nafasi ya Haruna
Moshi ambaye hayuko na Stars hapa baada ya kuumia mazoezini siku moja kabla ya
safari.
Kikosi
kamili cha Taifa Stars ambayo itatumia mfumo wa 4-4-2 ni kima ifuatavyo;
Kipa; Juma Kaseja
Mabeki; Shomari
Kapombe, Amir Maftah, Aggrey Morris na Kevin Yondani
Viungo; Shabani Nditi,
Salum Abubakari, Frank Domayo na Mwinyi Kazimoto
Washambuliaji; Mbwana Samata
na Mrisho Ngasa
Wachezaji
wa akiba; Mwadini
Ali, Waziri Salum, Juma Nyoso, Erasto Nyoni, John Bocco, Simon Msuva, Jonas
Mkude, Christopher Edward na Ramadhan Singano.
Kim
amesema kikosi chake kimejiandaa vizuri kwa ajili ya mechi hiyo, na kilichobaki
ni kwa wachezaji kudhibitisha maandalizi hayo kwenye dakika 90 za mchezo huo
utakaoanza saa 11 kamili jioni (nyumbani itakuwa saa 2 kamili usiku).
Mechi
hiyo itaoneshwa moja kwa moja (live) kupitia televisheni ya RTI ambapo
itaonekana katika nchi 58 duniani.
Mwamuzi; Slim Jedidi
(Tunisia)
Mwamuzi
msaidizi namba 1; Bechir
Hassani (Tunisia)
Mwamuzi
msaidizi namba mbili; Sherif
Hassan (Misri)
Mwamuzi
wa akiba; Youssef
Essrayri (Tunisia)
Mtathmini
wa waamuzi; Rachid
Medjiba (Algeria)
Kamishna
wa mchezo; Saleh
Issa Mahamat (Chad)
Friday, June 1, 2012
JUMAMOSI HII KUMJUA MREMBO ATAKAYEWAKILISHA MTWARA PALE MAKONDE BEACH CLAB
Warembo watakaopanda jukwani kushiriki katika shindano la kumtafuta Miss Mtwara 2012 siku ya jumamosi juni 2 katika ukumbi wa Makonde Beach mjini Mtwara, ambapo wamekuwa wakiendelea na mazoezi katika ukumbi huo kujiweka tayari kwa ajili ya shindano hilo.
Warembo watakaopanda jukwani kumtafuta Miss Mtwara 2012 Wakimsikiliza mkufunzi wao Isabela mpada (MISS RUVUMA 2006) siku ya jumamosi Juni2 katika ukumbi wa makonde beach
Warembo watakaopanda jukwani kumtafuta Miss Mtwara 2012 Wakimsikiliza mkufunzi wao Isabela mpada (MISS RUVUMA 2006),Pamoja na muandaaji wa shindano Rajab Mchatta. siku ya jumamosi Juni 2 katika ukumbi wa makonde beach
WABISOCO MKOANI MTWARA KUFANYA MKUTANO WA MWAKA KESHO
Chama cha ushirika wa wafanya biashara mkoani mtwara (WABISOCO) Kinatarajia kufanya mkutano wake mkuu wa mwaka wa chama hicho jumamosi hii katika ukumbi wa ushirika uliopo katika manispaa ya mtwara mkoani hapa
Akizungumza na Waaandishi wa ofisini kwake mapema leo Katibu wa Chama hicho Ndugu Hamza Licheta alisema kuwa katika mkutano huo utaambatana na kuchagua viongozi wapya watakaoongoza Chama hicho hapo baadae
Licheta ametoa wito pi kwa wafanya biashara waliowasnachama wa chama hicho kuhakikisha wanalipa ada ya uanachama wao ili waweze kushiriki katika mkutano huo vinginevyo mwanachama ambae hatolipa ada ya uanacahama wake hatoruhusiwa kuhudhurioa mkutano huo
Aidha ameongeza kuwaomba wananchama wa wabisoco mkoani mtwara kuhakikisha wanahudhutri kwa wingi ili kuweza kufanikisha mkunao huo kufanyika hapo kesho
Kufanyika kwa mkutano huo wa mwaka wa wabisoco kunakuja baada ya wanachama wa wabisoco kudai kufanyika kwa mkutano mkuu ambapo ulikuwa haujaitishwa kwa muda mrefu
Subscribe to:
Posts (Atom)


