Friday, October 4, 2013

Cocacola kufungua Studio



Kampuni ya vinywaji baridi ya Coca Cola imewaonyesha wadau mfululizo wa vipindi vya televisheni vya Coke Studio vilivyorekodiwa vinavyowahusisha wasanii wanaofanya vizuri barani Afrika.

Mfululizo wa vipindi hivyo vya televisheni, umetambulishwa rasmi jana usiku Jijini  ambapo baadhi ya washiriki, wasanii na wadau mbalimbali waliohudhuria kujionea kazi hiyo, katika uzinduzi huo uliopambwa na burudani ya muziki kutoka B Band.

Wadau waliohudhuria walipata nafasi ya kutazama sehemu ya kwanza ya kipindi kutoka Coke Studio, na eNewz ilikuwepo kufuatilia kwa karibu ambapo pia tulipata nafasi ya kuongea na wasanii washiriki walioiwakilisha Tanzania, Diamond pamoja na Lady Jay Dee ambao wamesema wamefurahi sana kupata nafasi hii kubwa ya kuendelea kuupanua muziki wao Afrika na duniani kwa ujumla.

Kwa upande wake, Meneja Bidhaa Coca Cola Tanzania Maurice Njowoka na amesema kuwa kampuni ya Coka Cola imejitoa kuwapatia nafasi watanzania hususan vijana nafasi ya kuendelea kunufaika na kufurahia burudani ya muziki pamoja na kuunganisha tamaduni za kiafrika.

Coke Studio Africa imeweza kuwaweka pamoja wasanii 24 wakubwa kabisa Afrika kutoka nchi 8 tofauti na kutengeneza nyimbo zipatazo 50 zilizowapagiwisha vilivyo wapenzi wa muziki. 

Tuesday, October 1, 2013

Dully awadiss Ney, Madee



Msanii Dully Sykes ambaye mitaa inasubiri kazi mpya kutoka kwake ambayo inakwenda kwa jina  Kabinti Special ambayo ataiachia rasmi mapema mwezi huu katika nafasi yake kama mkongwe wa sanaa ya muziki hapa Tanzania, ametoa maoni yake kuhusiana na wasanii wenzake wanaojiita Ma-rais.

Ujumbe huu mpya na mkali wa Prince Dully Sykes umeelekezwa haswa kwa wasanii Madee pamoja na Ney wa Mitego ambao kwa muda mrefu sasa wamekuwa na ubishi endelevu kati yao juu ya ni nani Rais wa Manzese ambapo ndipo wanapotokea.

Dully amesema kuwa anawashangaa sana wasanii hawa ambao amewataja kama wadogo zake kwa kugombania Urais hewa ambao hauna maslahi zaidi ya kulazimisha heshima wakati Tanzania kuna rais mmoja tu ambaye ni Rais Kikwete.

Kwa sasa tunaendelea kusuburi kwa hamu kusikia majibu ya Ma Rais hao wa muziki Madee pamoja na Ney wa Mitego ambao wanakalia kiti kimoja kuiendesha nchi ya kitongoji cha Manzese Jijini Dar es Salaam.

Afrika yang'aa kwenye tuzo



Kutoka katika orodha ya majina ya wasanii ambao wanawania tuzo za Black Entertainment Film Fashion Television and Arts za mwaka huu, wasanii wakali kabisa kutoka Afrika akiwepo Zahara, D Banj Petersen Zagaze, Jose Chameleone, Juliana pamoja na wengineo wameweza kungara kwa kutokezea katika vipengele mbalimbali.

Katika tuzo hizi ambazo hufanyika huko UK, zimewarudisha tena wasanii wa Uganda Juliana pamoja na Chameleone katika kipengele kimoja ambapo mwaka jana mwanamama Juliana ndiye aliyefanikiwa kuibuka mshindi.

Utaratibu wa kuanda kuwapigia kura wasanii wanaowania tuzo kwa njia ya mtandao ili kuwawezesha kushinda utaanza rasmi tarehe 6 mwezi Octoba, na maboresho yaliyofanyika yanatarajiwa kuongeza msisimko wa aina yake katika sherehe za tuzo hizo mwaka huu.

Dawa ya kutibu Virusi vya UKIMWI

Wakati madaktari wa nchi za wenzetu wakihangaika kutafuta muafaka wa magonjwa yanayotusumbua kwa kufanya utafiti na kuripoti nini kinaendelea hususa kuhusu suala la UKIMWI wa kwetu wako Kimya na kinyongo kikali kwa kunyimwa poshoz zao na kulipwa kiduchu, na kipigo juu yake. Hii ni sababu ya kuchanganya siasa na utaalam, japo siasa na yenyewe ni utaalam si vyema utaalam wake ukauingiza kwenye masuala muhimu kama afya.
Taarifa kutoka Rutgers New Jersey Medical School zinaeleza kuwa dawa aina ya Ciclopirox ambayo kwa muda mrefu ilikuwa ikitumika kutibu fangasi, ina uwezo wa kuzifanya Cell ambazo tayari zina virusi kujiharibu na hivyo kuondoa virusi hivyo. Kwa taarifa kamili na tafsiri sahihi soma mwenyewe hapo chini.

Angalizo: UKIMWI ni jamnga la Taifa hili. Naombeni uzi huu hapa ubaki ili Madaktari wetu waone hii wasome na watest kwenye maabara zao tuone kama taifa letu litapona. 

NEWARK, N.J. -- The topical anti-fungal drug Ciclopirox causes HIV-infected cells to commit suicide by jamming up the cells’ powerhouse, the mitochondria — according to a study by researchers at Rutgers New Jersey Medical School. And unlike current anti-HIV drugs, Ciclopirox completely eradicates infectious HIV from cell cultures, with no rebound of virus when the drug is stopped. The study has been published in the journal PLOS ONE.

The treatment of patients with HIV has been revolutionized by the advent of combination anti-retroviral drugs. But although these drugs are highly effective at keeping HIV at bay, they must be taken for the life of the patient and never eliminate the infection completely. This is illustrated by the often rapid resurgence of virus in patients who stop taking these medications. The persistence of HIV is partially due to the ability of the virus to disable the cell’s altruistic suicide pathway, which is normally activated when a cell becomes infected or damaged.

A team of researchers from three departments at New Jersey Medical School, led by Michael Mathews and Hartmut Hanauske-Abel, previously showed that Ciclopirox, commonly used by dermatologists and gynecologists to treat fungal infections, inhibits the expression of HIV genes in culture. The group now shows that the drug works against HIV in two ways: It inhibits the expression of HIV genes and also blocks the essential function of the mitochondria, thereby reactivating the cell’s suicide pathway. Healthy, uninfected cells examined during this study were spared. And remarkably, the virus did not bounce back when Ciclopirox was removed. 

The utility of Ciclopirox in patients with HIV, for instance after topical application to reduce sexual transmission of the virus, awaits verification in future clinical trials. However the fact that Ciclopirox is already approved for treatment of patients by the FDA and by its European counterpart, the EMA, and therefore considered safe for human use, may eliminate much of the time and expense ordinarily involved in the drug development process. 

Indeed, the authors note the speed with which a second FDA-approved drug believed to have promise in subduing HIV, Deferiprone, has moved directly from tests in culture to a phase I human trial conducted in South Africa, thanks to previously published results now reinforced by additional research in culture described in the current paper. 

Studies in animals were safely skipped, creating a model for rapid transition from drug effect in a plastic dish to drug effect in patients. In contrast to Ciclopirox, approved for topical use, Deferiprone is FDA- and EMA-approved for systemic use (in certain thalassemia patients with iron overload). The discovery that two drugs, each well-tolerated by patients when used as indicated, are deadly to HIV-infected cells, may open a new chapter in the fight against HIV/AIDS that moves the world closer to the eradication of HIV-1 infection. 

Established in 1766, Rutgers, The State University of New Jersey, is America’s eighth oldest institution of higher learning and one of the nation’s premier public research universities. Serving more than 65,000 students on campuses, centers, institutes and other locations throughout the state, Rutgers is the only public university in New Jersey that is a member of the prestigious Association of American Universities.

Rutgers Biomedical and Health Sciences (RBHS) is the health care education, research, and clinical division of Rutgers University, comprising nine schools and their attendant faculty practices, centers, institutes and clinics; New Jersey’s leading comprehensive cancer care center; and New Jersey's largest behavioral health care network.

Mcheki mwanaume anayejivunia kuwa na umbo la kike



Mcheki mwanaume kutoka nchini Nigeria mwenye muonekano na pozi za  kike na mwenye kupendelea mavazi ya yanayopendwa na kina dada
 Akifungukia muonekano wake Tosin Silver ambaye ni mwigizaji na mwanafunzi wa chuo,anasema anajivunia kuwa hivyo japo watu wanamfikiria kuwa yeye ni shoga.

"Najivunia kwa jinsi nilivyo..natakiwa kujipenda jinsi nilivyo..mwanzo nilikuwa nahuzuni kiasi kuhusiana na muonekano wangu ila sasa najivunia kwa sababu ndio Mungu alivyoniumba " Amesema Tosin.

Isome hapa post nzuri toka kwa Jay Dee dili kwa mabinti


Mwanamuziki anayefanya vizuri kitambo na mmiliki wa Machozi Band Lady Jaydee a.k.a Anaconda amefunguka kupitia ukurasa wake wa facebook kuwa ana mpango wa kutimiza ndoto za mabinti wenye vipaji.
'Kuna nafasi na kitu kizuri kinakuja kwa waimbaji wa kike.. Hivyo endelea kutembelea page hii kufahamu zaidi.Inaweza kuwa ndio nafasi yako kutoka na kuwa moja kati ya wanamuziki maarufu wa kike Tanzania.' ameandika Lady Jaydee kwa hiyo kaa mkao wa kula kwa mambo mazuri.


Pia Jide ametoa tahadhari kwa watumiaji wa mtandao wa facebook kuepuka matapeli wanaotumia jina lake kujipatia pesa.. 'Asanteni kwa kufika 90,399.. Naomba mnisaidie kusambaza ujumbe kuwa sina account yoyote ya facebook inayotoa mikopo. Saidia ndugu na jamaa wasitapeliwe. Hii ndio akaunti halali ya JIDE na si vinginevyo.. Jihadhari na wezi na muwe na siku njema pia...'

Monday, September 23, 2013

ICC yaahirisha kesi ya Ruto kwa wiki moja

William Ruto

Majaji katika mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC wameahirisha kesi ya naibu Rais wa kenya William Ruto kwa juma moja ili kumpa mda kurejea nyumbani kushughulikia hali ya kiusalama inayokumba taifa hilo.

Watu wanoaminika kuwa magaidi wa Al Shabaab wameteka jumba la kifahari lenya maduka la Westgate jijini Nairobi na kuwazuilia mateka wakenya kadhaa.

Bwana Ruto anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kibinadamu kufuatia ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007 nchini kenya.

Ruto na Rais Uhuru Kenyatta, wanakabiliwa na tuhuma za za uhalifu dhidi ya binadamu baada ya kudaiwa kuhusika na ghasia za kikabila baada ya uchaguzi wa mwaka 2007-2008 ambapo watu zaidi ya elfu moja waliuawa.

Mahakama iliakhirisha kesi baada ya kikao cha dharura kuitishwa huku upande wa mashtaka ukisema kuwa hauna pingamizi lolote ikiwa kesi zitaakhirishwa kwa muda mfupi.


HABARI HIZI KWA HISANI YA BBC SWAHILI

Mlipuko watoke katika jengo ambalo magaidi wa Al shabab wamewateka nyara wananchi

Huku hali ya mshikemshike ikiendelea kushuhudiwa katika jengo la Westgate lenye maduka, ufyatulianaji risasi umesikika ndani ya jengo hilo lenye maduka na mikahawa zaidi ya themanini.

Milio hiyo ilidumu kwa dakika tatu na kufuatiwa na moshi mkubwa juu ya jengo hilo. Hakuna taarifa kamili kuhusu kilichosababisha moshi huo.

Wapiganaji wa Al shabaab wamewateka nyara raia ambao idadi yao haijulikani.

Walikuwemo ndani ya jengo wakiendelea na shughuli zao kuanzia Jumamosi mchana wakati wapiganaji wa Al shabaab walipowavamia na kuanza kufyatua risasi kiholela.

Inaarifiwa kuna maiti kumi katika ghorofa ya kwanza ya jengo hilo.

Aidha wapiganaji hao wanaoaminika kuwa wanachama wa Al Shabaab ni kati ya kumi na kumi na watano na bado wangali ndani ya jengo hilo.

Ripoti zinasema kuwa ufyatulianaji mkubwa wa risasi pamoja na milipuko imesikika katika jengo hilo kwa takriban dakika 15.


Harakati za kuendelea kumaliza operesheni hiyo zinaendelea lakini hali ya mateka walio ndani ya jengo hilo inaendelea kudorora.

Tuesday, September 17, 2013

Shetta achukia baada ya kukaguliwa kama jambazi uwanja wa Ndege Zanzibar

Shetta na Chege wakikaguliwa Uwanja wa Ndege wa Zanzibar
Msanii Shetta ameonekana kukerwa na kitendo cha kukaguliwa begi lake  na kutoa kila kitu kilichokuwa ndani ya begi lake kwa ajili ya kukamilisha ukaguzi huo, katika uwanja wa ndege wa Zanzibar akisafiri kuelekea Mombasa akiwa na msanii mwenzake kutoka kiumeni "Chege"
Kutokana na matukio ya watanzania wengi kujihusisha na usafirishaji wa madawa haramu ya kulevya, serikali imekuwa makini sana kwa wasafiri wanaotumia usafiri wa anga kutoka na kuingia ndani ya nchi, kuhakikisha hakuna kila anaejihusisha na kazi hiyo kufikishwa katika mikono ya sheria.

Mcheki hapa Balozi wa China akiwa na Kofia ya CCM







Matokeo ya Mechi za UEFA yako hapa

Photo: Matokeo Champions League

DKT. Kawambwa azindua Mradi wa Maji Kunywa Kerege Bagamoyo

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt Shukuru Kawambwa (wa tatu kushoto) akikata kamba kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi ya kunywa katika shule ya msingi Kerege Bagamoyo

 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt Shukuru Kawambwa(katikati) akigonganisha vikombe na wanafunzi wa shule ya msingi Kerege Bagamoyo pamoja na Raisi wa Daressalaam Rotary Club,mwenye miwani bi Nadine Atallah kama ishara ya kufurahia huduma ya maji safi katika shule hiyo. Klabu hiyo ndio imeligharamia mradi huo.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt Shukuru Kawambwa(katikati) akinywa maji mara tu baada ya kuzindua mradi wa maji safi ya kunywa katika shule ya msingi Kerege Bagamoyo, kushoto ni Raisi wa Daressalaam Rotary Club bi Nadine Atallah. Klabu hiyo ndo wadhamini wa Mradi huo. Wengine ni wanafunzi wa Shule hiyo.

Tuesday, September 3, 2013

Urban Boys yapata Dili Ubelgiji



Ni kundi ambalo hivi sasa limekuwa likishika headlines mbalimbali Afrika Mashariki si wengine bali ni The Urban Boys kutoka nchini Rwanda Kigali ambao hivi sasa wamepata bonge moja la shavu la kusafiri kuelekea nchini Ubelgiji kutumbuiza katika tukio la kumtafuta Miss and Mister Rwanda/Belgium 2013.

Ni wiki chache zilizopita kundi hilo lilitangazwa kuwa washindi wa shindano kubwa la kutafuta nyota wa muziki nchini humo la Super Star Season Three ambapo mmoja wa memba wa kundi hilo anayeitwa Safi Niyibikora, aka Safi Lee, ameelezea kufurahi sana kupata nafasi hiyo ambayo itawapa fursa ya kuweza kujitangza zaidi kimataifa.


Shindano hilo linatarajiwa kufanyika huko Brussels, Belgium tarehe tano mwezi Oktoba mwaka huu huku ikiwa ndio mara yao ya kwanza kabisa kutumbuiza nchini humo na barani Ulaya japokuwa wamekuwa wakipata mashavu kadhaa ya kutumbuiza Afrika Mashariki.

Huyu Ndiye Ktibu Mkuu Mpya wa Yanga anayechukua Nafasi ya Mwalusako

Naggi

Anayetarajiwa kuchukua nafasi Lawrence Mwalusako ni Patrick Naggi amewahi kuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF).

Tayari Naggi ambaye aliwahi pia kuwa CEO wa Tusker ya  Kenya yuko nchini kumalizia mazungumzo na Yanga ili kuchukua nafasi na katibu mkuu Yanga.

Lakini taarifa zinasoma, Naggi aliwahi kufukwa kazi katika KFK kutokana na upotevu wa mipira 100.

Hata hivyo, mwenyewe aliwahi kulalamika kwamba mipira hiyo iliyotolewa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf) haikuwa katika kiwango hicho.


Aidha, Naggi aliwahi kulalamika kwamba hakupewa nafasi ya kujieleza kutokana na kilichotokea.

Mwalusako aachia Ngazi Yanga wanachama waitisha Mkutano na Waandishi wa habari leo



Katibu Mkuu Yanga, Lawrence Mwalusako ameamua kuachia ngazi baada ya kukaimu kwa mwaka mmoja.

Mwalusako amesema amefanya hivyo kwa kuwa makubaliano yao yalilikuwa ni kukaimu nafasi hiyo kwa mwaka mmoja.

“Haya ndiyo yalikuwa makubaliano yetu na sasa muda mwafaka umefika wa kufanya hivyo,” alisema hivi punde.

Lakini uchunguzi wa Blog hii umeonyesha kuwa Yanga imeleta Mkenya kuchukua nafasi yake hiyo na tayari ameanza kazi.

Mkenya huyo anajulikana kwa jina Patrick Naggi kuchukua nafasi hyo.


Taarifa hizo zinaaleza Naggi amewahi kuwa Technical Director wa Shirikisho la Soka la Kenya (KFF) na CEO wa Tusker ya  Kenya.